Aina za vitisho
Kitisho ni pale mtu anaposema au anapoonyesha anataka kukudhuru wewe au mali yako. Vitisho vinaweza kujumuisha madhara ya kimwili au kihisia, uharibifu wa mali yako, matusi, kujaribu kukutisha, au unyanyasaji.
Kuna aina tofauti za vitisho na njia za kushughulika navyo.
- Kitisho cha ana kwa ana hutokea pale ambapo mtu aliye karibu nawe anapoonyesha anataka kusababisha madhara.
- Kitisho kwa njia ya simu hufanywa kwa simu. Wakati mwingine vitisho vinavyotolewa kwa simu vinaweza kuwa "simu za mzaha". Hii ni wakati mtu anafanya utani na kitisho kinakuwa sio kweli. Mara nyingi ni bora kuichukulia kama kweli ikiwa huna uhakika.
- Kitishio cha ujumbe wa kielektroniki kawaida hupokelewa kupitia ujumbe wa maandishi, mitandao ya kijamii au barua pepe.
- Uhalifu wa chuki unahusisha vitisho au madhara yanayoelekezwa kwako kwa sababu ya rangi yako, dini, mwelekeo wako wa kingono, asili ya taifa, au utambulisho mwingine wa mtu binafsi.
Fahamu jinsi ya kujilinda mwenyewe dhidi ya wathibitisha na tovuti bandia. Jifunze nini cha kufanya unapokuwa mwathirika wa udanganyifu.
Jinsi ya kushughulikia kitisho
Kitu unachopaswa kukifanya kinategemena na aina ya kitisho na ukubwa wa kitisho hicho.
Kushughulika na kitishio cha ana kwa ana
- Usalama wako ni muhimu sana. Angalia haraka kila mahali na utafute mahali salama pa kwenda. Hapa kunaweza kuwa mahali penye shughuli nyingi na watu wengi au mahali unapoweza kujificha.
- Kuwa mtulivu. Epuka kutazamana machoni au kuongea na mtu anayekutishia. Onyesha lugha ya kawaida ya mwili na kimbia au rudi ulikotoka haraka.
- Piga simu 911 kwa msaada wa haraka.
- Omba msaada kutoka kwa watu ambao wanaweza kuwa karibu nawe.
- Ficha na ujaribu kuzuia njia inayokuja kwako. Nyamazisha simu yako.
- Jaribu kutambua maelezo kuhusu tukio hilo. Piga picha au video kama ni salama kufanya hivyo au umuombe mtu aliye karibu afanye hivyo. Ikiwa hujui mtu anayekutishia, tafuta vitu vya kusaidia kutambua mtu huyo kama umri wao, jinsia, rangi, urefu, uzito, nywele na rangi ya macho, nguo, na kitu kingine chochote kinachoonekana.
- Pigana tu kama ndiyo njia ya mwisho maisha yako yanapokuwa katika hatari ya haraka.
- Toa taarifa ya kitisho kwa watekelezaji wa sheria.
Piga simu 911 ikiwa wewe au mtu mwingine yuko katika hatarini. Fahamu nini cha kutarajia unapopiga simu polisi.
Kushughulikia kitisho kwa njia ya simu au kwa ujumbe
- Tulia na usikate simu. Jaribu kupata taarifa zaidi kuhusu mtu anayekutishia. Uliza maswali ili kukusaidia kujua ikiwa kitisho ni cha kweli.
- Usijibu ujumbe, machapisho ya mitandao ya kijamii, au barua pepe.
- Hifadhi taarifa. Weka ujumbe na uandike nambari ya simu au anwani ya barua pepe. Piga picha ya vitisho kwenye mitandao ya kijamii. Rekodi simu ikiwezekana au andika kile kilichosemwa mahususi. Andika hasa kile kilichosemwa. Unaweza kurekodi simu ikiwa ni halali katika jimbo lako.
- Mzuie mtu huyo baada ya kuhifadhi ushahidi.
- Toa taarifa ya kitisho kwa watekelezaji wa sheria.
Learn what to do if ICE comes to your home, job, or stops you in public. Understand your rights and how to make a safety plan.
Kujibu vitisho kutokana na hali yako ya uhamiaji
- Tumia Kiingereza katika hali hiyo ikiwezekana.
- Usihisi haja ya kuwaelimisha watu kuhusu imani zao potofu. Watu ambao wanafanyiwa ubaguzi wa rangi au vurugu hazina mantiki.
- Tafuta msaada wa kisheria ikiwa mtu anatishia kukuitia mamlaka za uhamiaji na unaogopa kufukuzwa nchini.
- Ripoti uhalifu wa chuki kwa polisi wa eneo husika au FBI.
- Wasiliana na mashirika ya haki za kiraia, hasa kama hujisikii vizuri kuzungumza na watekelezaji wa sheria.
- Pata maelezo kuhusu haki zako kama mhamiaji.
- Wasiliana na wanajamii wako. Kuzungumza juu ya vitisho na watu wengine ambao wamepitia mambo kama hayo inaweza kukusaidia kujua nini cha kufanya.
Baada ya kupata kitisho, jaribu kutafuta msaada wa kihisia. Ongea na mwanafamilia, rafiki, kikundi cha jamii, au mtoa huduma ya afya ya akili unayemuamini. Pata maelezo zaidi kuhusu huduma za afya ya akili.
Nini cha kufanya ikiwa unashuhudia mtu akitishiwa
- Zungumza au rekodi kitisho hicho kama ni salama kufanya hivyo.
- Piga simu 911 kama mwathiriwa wa kitisho yuko hatarini.
- Zungumza na mwathiriwa. Toa msaada na uulize jinsi unavyoweza kuwasaidia. Sikiliza matakwa yao kabla ya kuchukua hatua yoyote.
- Jitolee kuondoka na mwathirika.
- Kaa na mwathirika baada ya kitisho kama anahitaji msaada zaidi.
Toa taarifa ya kitisho
Ikiwa mtu anakutishia, unaweza kutoa taarifa polisi. Unaweza kupiga simu 911 wakati wa kitisho au kwa polisi wa eneo husika baada ya kitisho. Ikiwa hujisikii vizuri kupiga simu kwa polisi, kuna rasilimali zingine za usalama zinazopatikana kwako.
Kwa vitisho katika sehemu maalum, unaweza kuwajulisha wafanyikazi au waulinzi husika. Kwa mfano, ikiwa kitisho kinatokea kazini, zungumza na msimamizi wako au idara ya rasilimali watu. Ikiwa kitisho kinatokea kwenye basi, mwambie dereva wa basi.
Pia, unaweza kuwasiliana na mashirika haya kwa msaada unaohusu vitisho:
Contact | Kwa |
|---|---|
Vitisho kwenye haki zako za kiraia, ikiwemo haki za wahamiaji na LGBTQ + | |
Vitisho kwa haki za kiraia kwa Waafrika wa Marekani na uhalifu wa chuki | |
Vitisho kwa Wamarekani wa Asia | |
Vitisho kwa haki za kiraia za Waislamu na uhalifu wa chuki | |
Vitisho kwa jamii za LGBTQ + | |
Vitisho katika nyumba yako | |
Ofisi ya FBI ya eneo husika (800) 225‐5324 | Vitisho vya mawakala wa serikali za kigeni, maafisa wa serikali, uhalifu uliopangwa, na uhalifu wa chuki |
Vitisho kwenye mitandao ya kijamii |
Je, ninaweza kuripoti tishio bila kujulikana?
Ndiyo, unaweza kuripoti tishio bila kutaja jina lako, lakini kwa njia fulani tu.
- Simu kwa 911 na kwa polisi wa eneo lako SI za siri: Wahudumu wa simu za 911 na vituo vya polisi wa eneo husika huona nambari yako ya simu na mahali ulipo moja kwa moja.
- Piga simu za dharura huru: Baadhi ya programu, kama vile Crime Stoppers (1-800-222-8477) na WeTip (1-800-782-7463) huruhusu ripoti bila kujulikana.
- Tumia fomu za vidokezo mtandaoni: Unaweza kuwasilisha vidokezo kupitia polisi wa eneo lako au tovuti za FBI. Acha tu sehemu za jina na anwani ziwe wazi kabisa.
Idara nyingi za polisi haziulizi kuhusu hali ya uhamiaji, lakini sera hutofautiana kulingana na eneo. Ikiwa una wasiwasi, wasiliana na mtoa huduma wa kisheria au mojawapo ya mashirika ya utetezi yaliyoorodheshwa hapo juu.
Fahamu jinsi ya kupata msaada wa bure au wa gharama nafuu kutoka kwa wanasheria wa uhamiaji wanaoaminika.
Nini kitatokea baada ya kuripoti tishio?
Kila shirika lina taratibu tofauti za kuchunguza na kushughulikia vitisho. Wasiliana na shirika lako kuhusu hatua zinazofuata.
Kwa kawaida, polisi huchunguza tishio hilo na mtu aliyetoa tishio hilo. Ukipiga picha au video, hizi zinaweza kutumika kama ushahidi. Ikiwa polisi watagundua kuwa tishio hilo ni la kuaminika na ni ukiukaji wa sheria, wanaweza kukamata na kupeleka kesi hiyo kwa waendesha mashtaka. Kutishia kuumiza mwili ni kosa kubwa katika majimbo mengi.
Unaweza pia kufungua kesi ya madai katika mahakama ya eneo lako kwa madhara ya kihisia au ya mwili. Unaweza kuwasilisha ombi la amri ya kumzuia mtu fulani ili aache kukutishia na kukaa mbali nawe.
Zaidi kutoka USAHello
Je, unatafuta taarifa mahususi?
Taarifa kwenye ukurasa huu inatoka USA.gov, the FCC, na vyanzo vingine vinavyoaminika. Tunakusudia kutoa taarifa rahisi kueleweka ambazo zinarekebishwa mara kwa mara. Taarifa hii sio ushauri wa kisheria.